Tuesday, February 9, 2010
UNAPOTOKA OUT NA MUMEO HALAFU YUPO NA MARAFIKI ZAKE,UNAJISIKIAJE?
Kuna siku nilikuwa nimepita mahali nikawa nimekaa namsubiri mtu,sasa pembeni yangu kulikuwa na meza ambayo wamekaa wanaume 7.Baada ya muda akaja jamaa ameongozana na mwanamke akawa amefika katika ile meza akawa anawaambia wale majamaa 7 kuwa ametoka leo ameamua kuja pale na wife...majamaa wakamkaribisha shemeji yao na kuhakikisha anapatiwa huduma zote.Sasa kilichoendelea ni kwamba yule dada akawa hayupo sehemu ya mazungumzo pale.Wale wanaume wakaanza kuongea mambo yao ya mpira,siasa na mengine ya kikazi.Dada wa watu akawa anachezea tu simu yake na kucheka kidogo na kuongea mara chache pale anapoweza kuongea lakini kwa kumtazama alikuwa bored.
Sasa leo kwenye leo tena nikahoji hali kama hii inapokutokea umetoka na mpenzi wako lakini huko anakutana na marafiki zake 3 au 4 mnakaa na kujumuika nao wewe unakuwa katika hali gani?unaenjoy?
MSG zilizoingia baadhi:
1.Kwa mimi sitajisikia vizuri maana nitaboreka na maongezi yao maana mengi yatakuwa hayanihusu nitakuwa kama bendera fata upepo...Tunu.
2.Mimi nilitoka siku moja na mume wangu mpaka ilibidi nimtumie msg kumwambia tuhame maana alinitelekeza kama sipo maana sikuwa sehemu ya maongezi yao...Raya
3.Mie nafurahi maana napata muda wakuwajua mashemeji zangu.
4.Kutoka na mpenzi na marafiki inapoteza ule uhalisia wa couple outing,maana mimi kama mimi ntakuwa siongei maana ukiongea sana hawachelewi kusema hujatulia,ukinyamaza kwa heshma watasema unapozi basi tabu tupu.
Mie nikasema kuwa sawa ni raha kutoka na mpenzi wako na kumuona kiuhalisia anavyokuwa nje na marafiki zake unakuwa unamsoma na kumjua..lakini pia kama mmepanga kutoka na ikatokea umekutana na marafiki zako waambie jamani mie nipo ila leo nipo na mpenzi wangu then kuwa na time na mpenzi wako muongee ya kuongea na kuenjoy pamoja maana ndio kilichowatoa nyumbani.Hayo yalikuwa yangu na tunaweza kuliangalia hili kwa mawazo tofauti hivyo ndio mimi nafikiri.
Monday, February 8, 2010
KURUNDIKA CHUPI HALAFU ZIKIJAA BAADAE NDIO UZIFUE NI SAHIHI?TUNAEZA ITA NI UCHAFU?AU TUITEJE?AU NI SAWA KUNA FAIDA

Dina mambo,
Kuna hii issue ambayo katika Radio unayofanya kazi naona mambo mengi pia mnadiscuss humo ,ningependa uijadili ili watu wahusika wapate kweli yao."ni kuwa kuna Tabia au Hulka ya wadada wengi kuwa na taratibu za kuvaa nguo za ndani (Chupi.. unisamehe hapo) kutaja moja kwa moja...na wakivua wanahifadhi na kuchukua nyingine,na unakuta mtu hafui hapo hapo..anarundika labda wiki moja au mwingine mwezi...na baada ya hapo analoweka zote chafu sasa na kufua...,mie huwa nachukia hii tabia kwa wanawake wenzangu,kwani haipendezi...uongelee hili swala katika blog yako ata radio kama itawezekana,sidhani hizi nguo za ndani zinafaa uweke kama nguo chafu...ukirundika"
Wadau tusaidiane katika hili,mwenzetu kauliza
JANA NILIKUTA UJUMBE HUU PALE SAMAKI SAMAKI NIKAUFIKIRIA KWA MAKINI NA KUUTAFAKARI KIUKWELI NILICHEKA SANA
JUMAPILI USIKU,NILIKUWA NATEMBEA TU MAENEO YA MJINI KUMBE RAHA SANA.
Tukafika mtaa wa samora kwenye bustani tukakaa na kupiga story,ilikuwa ni usiku wa saa sita watu wamelala mjini kumejaa walinzi tu na watu wachache sana wanaorudi majumbani mwao au kutoka na magari yao,yaaani nilienjoy kuliko kwenda kwenda disco ilikuwa ni kutembea tu
Sunday, February 7, 2010
MIZUNGUKO YANGU SIKU YA JUMAMOSI...
Nilikutana na huyu dada ambae alifurahi sana kuniona na kunifahamu maana amekuwa msikilizaji wangu mzuri kupitia leotena tukaongea ya kuongea basi na kufahamiana.
Friday, February 5, 2010
HAPPY BIRTHDAY MY BROTHER GERALD HANDO...
Leo tarehe 5 january mfanyakazi mwenzangu,rafiki yangu na kaka yangu Gerald Hando ambae anasikika kila siku asubuhi saa kumi na mbili alfajiri mpaka saa tatu katika Power Breakfast ni siku yake ya kuzaliwa.Kwangu mie nakupa pongezi nyingi na kukuombea maisha marefu, afya njema,kila siku endeleza ufanisi katika kazi yako,kuwa mwenye furaha kama kawaida yako.Ni mengi ningependa kukuwish ila kubwa zaidi mtangulize mwenyezi Mungu katika kila jambo lako.Happy Birtday to you my brada..
The secret of staying young is to live honestly, eat slowly, and lie about your age. ~Lucille Ball
The secret of staying young is to live honestly, eat slowly, and lie about your age. ~Lucille Ball
EVENT YA REDDS HAPO JANA PALE SAVANNA LOUNGE
Mie na Khadija MwanambokaThursday, February 4, 2010
USWAHILINI HATA JAMBO LA HATARI LINAWEZA KUWA KAMA SHEREHE...HAHAHAHAH
Hapa ni nyumbani kwa shosti aliyekuwa amefatwa kwa ajili ya kusutwa lakini baada ya kutonywa juu ya kasheshe ya msuto akawa ameingia mitini na kuitelekeza nyumba yake kama hivyo kwa hiyo wasutaji wakabaki kutukana nje na kupiga tarumbeta na kucheza baadae wakaondoka...hayo ndio mambo kila jambo laweza kuwa shughuli hahahahahah!
Kama vipi sikiliza leo tena kesho na mie Dina Marios.... katika hekaheka na Gea Habib utayajua vyema yaliyojiri.
Wednesday, February 3, 2010
KWA STYLE HII UMELALA NDANI MWENYEWE UNAJUA NJE KUNA MLINZI ANAKULINDA DUUH....
Jana mida ya saa sita usiku nilikuwa napita mitaa fulani hapa Dar es salaam,nikafika nyumba flani ambayo wenyewe kwa wakati huo walikuwa wamelala ndani kimyaaaaa lakini wakiwa na matumaini kuwa wapo salama kwani nje kuna mlinzi.Lakini bwana(mmasai) huyu alikuwa kwa nje akiuchapa usingizi ile kisawasawa kama nilivyoweza kumpata...kazi kweli kweli halafu mwisho wa mwezi unamlipa kwa kazi nzito anayoifanya ya kukulinda usiku wewe na mali zako.
Tuesday, February 2, 2010
JANA NILIPATA MARAFIKI WAPYA JAMANI....
KUOSHA MACHANUO NA VITANA NI MUHIMU PIA

Ni kawaida pindi tunapochana nywele kwa kutumia chanuo au vitana kuvihifadhi na kuendelea kuvitumia pasipo kuvisafisha.Wengi tunakumbuka kutoa nywele tu basi kwenye kitana au chanuo. Lakini la msingi kumbuka kuvisafisha hasa kuviloweka katika maji ya moto mara kwa mara na sabuni ili kuyeyusha mafuta yanayokuwa yameanda katika vitana husika si mafuta tu bali hata uchafu unaokuwepo kama mba na ngozi zilizokufa.
DUNIANI KILA MTU ANA MATATIZO YAKE....

Kama umesikiliza hekaheka ya leo unawezakuwa umeshangaa lakini ni kweli,kuna kaka anakaa Kigamboni vijibweni huyu kaka anaumwa anatatizo la kula na kusikia njaa kila wakati...ana tatizo hilo kwa miezi mitano sasa anaumwa hana nguvu na anasikia njaa kila wakati.
MLO...
Kila siku anakunywa uji chupa 13 chupa inayoingia vikombe kumi na mbili ,wali kilo 3, ugali kilo moja na nusu maji vidumu 5 vya lita 5...huo ni mlo wa siku nzima masaa 24 mpaka usiku analala anaamka kula kwa njaa anayokuwa nayo...hajui anaumwa nini maana hajaenda hospitali na hana pesa ya kwenda hospitali.Anaomba msaada wa chakula na matibabu.Tunampeleka katika njia panda jumapili aweze kupelekwa hospital kupata matibabu.
Monday, February 1, 2010
ASANTE WATANZANIA KWA KUMSAIDIA HUYU MAMA KUPITIA LEO TENA...
Hapa ni jana alikuwa amekuja ofisini maana kuna pesa ambayo niliifata CRDB bank kwa dada mmoja anaitwa Daina ambayo alijitolea kama msaaada kwa ajili yake.Kiukweli kina mama wengi baada ya kusikia habari ya huyu dada walijitolea sana kumpa mavazi,chakula,nguo zake na watoto,pesa,sabuni na maengine mengi na wengine kujitolea kumpa kazi ambayo atakuwa anafanya ili kujishughulisha.
Sunday, January 31, 2010
JAMANI NILIKUWA NAUMWA..........
Friday, January 22, 2010
HUU NI MFANO TU..........
Thursday, January 21, 2010
MPANGO MZIMA WA KUSHONEA WEAVING MUONE SANDRA......
MTEMBELEE MAMA TRACY PIA KATIKA BLOG YAKE..
mambo dina...
MIMI MAMA TRACYmsikilizaji mahili wa kipindi cha leo tena na nimchangiaje mzuri wa blog yako, nakupenda nakufagilia sana. ssa mpenzi, namimi nimefungua blog yangu, ambayo ni www.beautytouchdar.blogspot.com
itangaze kupitia blog yako ili waitambue. mambo kushirikiana dina au sio???asante kwa ushirikiano
Wadau mwenzutu nae ana mambo anataka kukupa mtembelee hapo.
MIMI MAMA TRACYmsikilizaji mahili wa kipindi cha leo tena na nimchangiaje mzuri wa blog yako, nakupenda nakufagilia sana. ssa mpenzi, namimi nimefungua blog yangu, ambayo ni www.beautytouchdar.blogspot.com
itangaze kupitia blog yako ili waitambue. mambo kushirikiana dina au sio???asante kwa ushirikiano
Wadau mwenzutu nae ana mambo anataka kukupa mtembelee hapo.
SINA MAPENZI TENA NA MKE WANGU...

Leo nimetumiwa msg na kaka mmoja wa Mwanza akiniomba nimshauri jambo,anasema ana mkewe wapo ndoani kwa miaka 2 lakini hana mapenzi na mkewe hampendi tena.Nikamuuliza kisa nini anasema hana sababu na wala hakulazimishwa kumuoa alimuoa akiwa na mapenzi nae kabisa lakini siku hadi siku mapenzi yamekuwa yakipotea mpaka sasa mwaka wa 2 hana mapenzi nae kabisa.Akaniomba nimshauri la kufanya...mimi nilichomuomba anipe mlolongo mzima wa maisha yao ya ndoa labda kuanzia hapo ndio naweza kujua nini kilitokea mpaka akamkinai mwenzake maana sina hakika akawa hana sababu maalumu sababu ipo ila yeye hajaiweka kichwani kama ndio sababu akiniambia ndio nitajua nimshauri nini maana kiukweli ni pazito.Labda kama wenzangu mna lakusema???
Wednesday, January 20, 2010
SASA HIVI HAKUNA VISINGIZIO TUMEEKIEWA MPAKA MASHINE KWENYE VYOO VYA BAR...
Tuesday, January 19, 2010
INASEMEKANA HARUFU YAKO YA MWILI INAWEZA KUMVUTIA MWANAUME...
Sahau kuhusu perfume......
Chuo kimoja cha maswala ya Saikolojia nchini Uingereza kimebainisha kuwa mwanamke unaweza kumvutia mwanaume kwa harufu yako ya asili ya mwili pasipo kujipaka manukato ya aina yoyote.Inasemekana kipindi cha ovulation(kupevuka mayai kabla ya kwenda hedhi) ndio kipindi mwanamke unakuwa na kiharufu fulani cha mwili ambacho mwanaume huvutwa....haya basi kina dada tukae bila manukato kipindi hiki halafu tuone itakuwaje...lol.
Chuo kimoja cha maswala ya Saikolojia nchini Uingereza kimebainisha kuwa mwanamke unaweza kumvutia mwanaume kwa harufu yako ya asili ya mwili pasipo kujipaka manukato ya aina yoyote.Inasemekana kipindi cha ovulation(kupevuka mayai kabla ya kwenda hedhi) ndio kipindi mwanamke unakuwa na kiharufu fulani cha mwili ambacho mwanaume huvutwa....haya basi kina dada tukae bila manukato kipindi hiki halafu tuone itakuwaje...lol.
Monday, January 18, 2010
HILI NALO TULIANGALIE...............
Kuna dada nilikutana nae siku ya jumamosi ana alama kibao za kuvilia damu mwilini kama kapigwa.Kiukweli nilishindwa kuvumilia nikaamua kumuuliza mwenzangu mbona hivyo kuna nini?huyo dada akaanza sasa kunieleza.
Akasema amepigwa na mumewe siku ya ijumaa,kisa alikuwa mahali anakunywa sasa kuna kaka akakutana nae akawa anamtongoza wakabadilishana namba za simu.Sasa bidada akarudi nyumbani akiwa amelewa akaenda kulala na mumewe.Usiku sana wamelala na mumewe yule kaka aliyekuwa anamtongoza akaanza kupiga simu,bidada usingizi wa pombe hasikii simu mumewe akaamka akapokea simu.Kupokea simu yule kaka anamwambia mume mpe simu mwenye simu nataka kuongea nae,mume akamjibu mimi mumewe kuna maagizo yoyote maana mke wangu kalala.Yule bwana mpiga simu akasema mie huyo mpenzi wangu duuuh mume akakata simu huku mke anakoroma kachukua mkanda akaanza kumtandika ndio bidada kushtuka usingizini kipigo kikawa kipigo.Ikibidi amwambie mumewe yule kaka alikutana nae akawa anamtongoza.Nikampa pole sana maana kiukweli alikuwa amevilia damu na yeye ni mweupe,alichonishangaza hakuvaa nguo ya kumziba ili alama zisionekane kajiacha hivyo hivyo kavaa nguo ya mabega wazi.
Sasa mimi najiuliza wewe kama mke wa mtu kwa nini unagawa namba yako ya simu hovyo?
Ok sawa umetoa namba kwa nini usimwambie huyo bwana kuwa umeolewa na asikupigie simu hovyo hasa nyakati za usiku mumeo anakuwepo?wote hatupo wakamilifu lakini tunafanyaje kuepuka matatizo kama hayo?
Akasema amepigwa na mumewe siku ya ijumaa,kisa alikuwa mahali anakunywa sasa kuna kaka akakutana nae akawa anamtongoza wakabadilishana namba za simu.Sasa bidada akarudi nyumbani akiwa amelewa akaenda kulala na mumewe.Usiku sana wamelala na mumewe yule kaka aliyekuwa anamtongoza akaanza kupiga simu,bidada usingizi wa pombe hasikii simu mumewe akaamka akapokea simu.Kupokea simu yule kaka anamwambia mume mpe simu mwenye simu nataka kuongea nae,mume akamjibu mimi mumewe kuna maagizo yoyote maana mke wangu kalala.Yule bwana mpiga simu akasema mie huyo mpenzi wangu duuuh mume akakata simu huku mke anakoroma kachukua mkanda akaanza kumtandika ndio bidada kushtuka usingizini kipigo kikawa kipigo.Ikibidi amwambie mumewe yule kaka alikutana nae akawa anamtongoza.Nikampa pole sana maana kiukweli alikuwa amevilia damu na yeye ni mweupe,alichonishangaza hakuvaa nguo ya kumziba ili alama zisionekane kajiacha hivyo hivyo kavaa nguo ya mabega wazi.
Sasa mimi najiuliza wewe kama mke wa mtu kwa nini unagawa namba yako ya simu hovyo?
Ok sawa umetoa namba kwa nini usimwambie huyo bwana kuwa umeolewa na asikupigie simu hovyo hasa nyakati za usiku mumeo anakuwepo?wote hatupo wakamilifu lakini tunafanyaje kuepuka matatizo kama hayo?
Subscribe to:
Posts (Atom)
