TAFUTA HAPA

Loading...

MTWARA SIO SALAMA

Baada ya Waziri wa Nishat ikusoma hotuba yake.Mwishoni amesema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar hapo ndio vurugu zilipoanza.
Huko MIKINDANI ofisi zote za serikali zavamiwa na kuchomwa na mpaka daraja la Mikindani nalo limevunjwa kwa maana hauwezi kutoka wala kuingia MTWARA 
  • Kuna madai kwamba silaha zimeibiwa (Haijathibitishwa) 
  • Maaskari wanafanya msako wa nyumba hadi nyumba maeneo ya Magomeni na Mangowela
  • Askari achomwa mshale. Haijulikani hali yake
  • Ni mapambano baina ya vijana na maaskari. Vijana hawaogopi tena risasi wala mabomu . Kundi limeelekea Shangani kwenye nyumba za vigogo.
  •  Nyumba ya kupumzikia wageni inayoitwa Shengena Lodge imechomwa moto kwa kile kinachoelezwa kwamba iliwapokea askari Polisi.
  • Ofisi ya CCM saba saba imechomwa moto, na baadhi ya waandishi wamezingirwa maeneo ya Sokoni, sasa ni milio ya risasi na mabomu.
  • Matairi  kila  kona  ya mji  yamechomwa  barabarani  polisi  na  zimamoto   wanafanya kazi ya kuzima na kufukuza wananchi. Kauli mbiu "Gesi haitoki hata kwa bomba la peni"
  • Kambi ya Upinzani yaukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi
  • Nyumba kadhaa  za watumishi  wa Serikali  zimechomwa  maeneo ya Shangani.(habari haijathibitishwa rasmi)
  • Ni magari ya FFU tu ndio yapo barabarani nayo hupata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo yaliyowekwa na vijana,baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari eti kwakuwa walipita jirani na gari yao,askari wengi waliokuja si wa hapa Mtwara wengi wametoka Masasi na Lindi. Ving'ora vinalia ovyo ovyo.
  • watoto wamefungiwa mashuleni walimu wamekimbia
  •  Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara . Takriban mabomu 20 na ushee mpaka sasa. Na wanaendelea kupiga mabomu.
  • Sasa hali si shwari kila eneo, wakionekana watu watatu wanaongea maongezi maaskari wanapiga mabomu. Mabavu yamechukua mkondo wake. Wananchi wamejifungia majumbani mwao. Chuki dhidi ya Polisi yaimarika. Polisi wanapiga mabomu bila mwelekeo.
  • Magomeni na sokoni kimenuka, mabomu yanarushwa na wananchi wanakimbia ovyo.
  • Kituo  kimoja  cha habari  kinachorusha habari za bunge chazuia mawimbi yake kwa Mkoa wa Mtwara hivyo hakisikiki(Redio na TV). Na kimewanyima haki wananchi wa Mtwara ya kupata taarifa.(Hatimaye wamerejesha matangazo yao)
  • Maduka yote yamefungwa, baa zimefungwa, hakuna huduma za usafiri, ofisi za serikali zimepwaya kimsingi hakuna lolote linalofanyika
  • Boda boda zinazoonekana maeneo ya Nkanaledi na abiria zinapigwa mawe.
  • Makachero nao wanajifanya madereva wa boda boda na Bajaji, Tax wengine wanatembea na magari ya Serikali.
  • Maeneo yote yametawaliwa na ukimya.
Habari kwa hisani ya www.mtwarakumekucha.blogspot.com

TUMSAIDIE KIMAWAZO JAMANI MUME KAWA MCHUNGU!!

Dina naomba uniulizie kwa walimwengu niko kwenye kipindi kigumu cha maisha ambacho sijawahi kuishi.Nina mume wa ndoa na watoto wawili. mtoto wa kwanza nilizaa na mwanaume mwingine maisha ya utotoni  nilivyomaliza form six,baada ya hapo nilienda chuo nikaolewa na huyu kaka ambaye naye ana mtoto mmoja wa kike. 
Kinachotokea ni kwamba kila mwanangu anachokifanya anasema eeh kachukua kwa baba yake miye nakaa kimya ana taka mtoto nimbadilishe jina nimwite jina la ukoo wangu miye, ninavyoondika huu ujumbe kanipiga kisa jina hilo hilo na isitoshe ni mume jina tu mambo ya kanisani nalea watoto wangu mwenyewe nawasomesha hana anachonipa ananitukana kila mara miye mchawi eti namroga hapati kazi ana kama mwaka sasa hana kazi hana shukrani. 
 
Hivi ndoa kama hii nikiondoka walimwengu siwatanisema vibaya? kwasababu mtoto wangu wa kwanza ana baba mwingine nimechoka kupigwa kutukanwa kuonewa. akilewa anasifia wanawake zake wa zamani walikuwa wazuri baadaye anasema ni pombe kweli haya maisha jamani nipeni ushauri nimechoka jamani na hii ndoa bora nijikalie mwenyewe na kazi yangu ndio iwe mume wangu.

NAMNA MONIQUE ALIVYOPUNGUA UZITO!

Kwa miaka mingi nimekuwa shabiki wa Monique, Monique Angela Hicks msanii wa filamu na comedy wa Marekani.Baadae nikaanza kumfatilia na talk show yake ya the Mo'Nique show ambayo sikuipenda hakunifurahisha kwa kweli.Nampenda kama muigizaji na comedian baasi.
Kwa miaka yote namfatilia kama mwanamke mnene kweli kweli ikawa kama identity yake.Toka kwenye vichekesho vya the parkers kwa wale mnaovikumbuka alikuwa kibonge.
 Amecheza movies kibao niipendayo zaidi hizi ya Phat girls,Welcome Home Roscoe Jenkins,Two Can Play That Game,Precious filamu iliyompa tuzo nyingi sana mwaka 2009 na zingine kibao.
 Monique akiwa na mumewe Sidney Hicks ambae wamefahamiana toka wadogo wakiwa na miaka 14.Kabla alikuwa ameolewa alipoachika ndio akaoana na Hicks.Ndoa ambayo wao wanaiita open marriage 'hakuna siri'
Ikitokea umeona mtu mmetamaniana hakuna siri hata kama mmefaya tendo ukweli mezani maisha yanaendelea.Hakuna kuachana kisa mmoja ametembea na mtu nje ya ndoa duhhh!
Kwa muda sijamuona kwenye movies au popote hata talk show yake ilisimamishwa BET.Na mara ya mwisho kumuona alikuwa kapungua kiasi kutoka ule unene wake wa zamani.
Majuzi zimetoka picha zake akiwa kapungua sanaa hata ningeulizwa ni nani nisingemtambua.Sijui kwa nini nilikuwa nampenda alipopungua kidogo tu.Siri yake kubwa ni kula vizuri kwa afya na mazoezi ya nguvu.

WALE WAPENZI WA MOVIES ANGALIA NA HIZI KAMA HUJAZIONA!


Hii movie ni nzuri sana sitaki kusimulia wewe nenda kainunue uangalie mwenyewe.Ni movies wameigiza Bradley Cooper na Zoe Saldana mwanadada aliyetamba kwenye Avatar na Colombiana.
The place beyond pines.Wameigiza Ryan Gosling,Bladley Cooper na Eva Mendes.Katafute ziangalie hii ni mpya kabisa ya mwaka huu.
Zote zinaburudisha na kufundisha kitu kuhusu maisha haya tunayoishi kila siku.Ningependa kina baba muangalie hii zaidi kuliko hata wanawake.Athari za baba kutokuwa karibu na mtoto wa kiume katika kumlea.
Athari zinakuja kujitokeza akiwa mkubwa.Unadhani watoto wa kiume ni strong kihisia?sio kweli.Wenyewe hawalii lakini sauti zao za kulia huonekana katika matendo yao.Mtoto anaweza kuwa mwizi,mvuta bangi,kuvuta madawa ya kulevya hata kuwa jambazi,mtukutu hasikii kisa hakupata enough atention kutoka kwa baba.
Baba hakuwepo wala hakuwa good role model kwa kijana wake si kwa tajiri wala maskini.Baba unaweza kumpa mwanao kila kitu hasa wenzetu matajiri lakini kama haupo pale kihisia upo busy kusaka mahela ni kazi bure.

MAISHA

MIMI NA WEWE