Tuesday, February 9, 2010

MAMBO YA VALENTINE,PALE MZALENDO

UNAPOTOKA OUT NA MUMEO HALAFU YUPO NA MARAFIKI ZAKE,UNAJISIKIAJE?

Kuna siku nilikuwa nimepita mahali nikawa nimekaa namsubiri mtu,sasa pembeni yangu kulikuwa na meza ambayo wamekaa wanaume 7.Baada ya muda akaja jamaa ameongozana na mwanamke akawa amefika katika ile meza akawa anawaambia wale majamaa 7 kuwa ametoka leo ameamua kuja pale na wife...majamaa wakamkaribisha shemeji yao na kuhakikisha anapatiwa huduma zote.Sasa kilichoendelea ni kwamba yule dada akawa hayupo sehemu ya mazungumzo pale.Wale wanaume wakaanza kuongea mambo yao ya mpira,siasa na mengine ya kikazi.Dada wa watu akawa anachezea tu simu yake na kucheka kidogo na kuongea mara chache pale anapoweza kuongea lakini kwa kumtazama alikuwa bored.

Sasa leo kwenye leo tena nikahoji hali kama hii inapokutokea umetoka na mpenzi wako lakini huko anakutana na marafiki zake 3 au 4 mnakaa na kujumuika nao wewe unakuwa katika hali gani?unaenjoy?
MSG zilizoingia baadhi:
1.Kwa mimi sitajisikia vizuri maana nitaboreka na maongezi yao maana mengi yatakuwa hayanihusu nitakuwa kama bendera fata upepo...Tunu.
2.Mimi nilitoka siku moja na mume wangu mpaka ilibidi nimtumie msg kumwambia tuhame maana alinitelekeza kama sipo maana sikuwa sehemu ya maongezi yao...Raya
3.Mie nafurahi maana napata muda wakuwajua mashemeji zangu.
4.Kutoka na mpenzi na marafiki inapoteza ule uhalisia wa couple outing,maana mimi kama mimi ntakuwa siongei maana ukiongea sana hawachelewi kusema hujatulia,ukinyamaza kwa heshma watasema unapozi basi tabu tupu.
Mie nikasema kuwa sawa ni raha kutoka na mpenzi wako na kumuona kiuhalisia anavyokuwa nje na marafiki zake unakuwa unamsoma na kumjua..lakini pia kama mmepanga kutoka na ikatokea umekutana na marafiki zako waambie jamani mie nipo ila leo nipo na mpenzi wangu then kuwa na time na mpenzi wako muongee ya kuongea na kuenjoy pamoja maana ndio kilichowatoa nyumbani.Hayo yalikuwa yangu na tunaweza kuliangalia hili kwa mawazo tofauti hivyo ndio mimi nafikiri.

Monday, February 8, 2010

KURUNDIKA CHUPI HALAFU ZIKIJAA BAADAE NDIO UZIFUE NI SAHIHI?TUNAEZA ITA NI UCHAFU?AU TUITEJE?AU NI SAWA KUNA FAIDA


Dina mambo,

Kuna hii issue ambayo katika Radio unayofanya kazi naona mambo mengi pia mnadiscuss humo ,ningependa uijadili ili watu wahusika wapate kweli yao."ni kuwa kuna Tabia au Hulka ya wadada wengi kuwa na taratibu za kuvaa nguo za ndani (Chupi.. unisamehe hapo) kutaja moja kwa moja...na wakivua wanahifadhi na kuchukua nyingine,na unakuta mtu hafui hapo hapo..anarundika labda wiki moja au mwingine mwezi...na baada ya hapo analoweka zote chafu sasa na kufua...,mie huwa nachukia hii tabia kwa wanawake wenzangu,kwani haipendezi...uongelee hili swala katika blog yako ata radio kama itawezekana,sidhani hizi nguo za ndani zinafaa uweke kama nguo chafu...ukirundika"



Wadau tusaidiane katika hili,mwenzetu kauliza

JANA NILIKUTA UJUMBE HUU PALE SAMAKI SAMAKI NIKAUFIKIRIA KWA MAKINI NA KUUTAFAKARI KIUKWELI NILICHEKA SANA

Bonge la mkwara...sasa sijui huwa unafanya kazi huu mkwara....

JUMAPILI USIKU,NILIKUWA NATEMBEA TU MAENEO YA MJINI KUMBE RAHA SANA.

Jana jumapili mida ya saa moja usiku kuna mtu akanipigia simu kuniomba tutoke mitaa ya town akanionyeshe kitu tofauti.Basi na mie nikaitika wito tukaenda kula mishikaki mjini mtaa wa kitumbini ni mishikaki midogomidogo flani hivi inaliwa na kitu kinaitwa Hajam au mkate wa ufuta ila unafanana na chapati unatia na chachandu kwa utamu zaidi.Na wachoma mishikaki hao ni wasikilizaji wangu wazuri kupitia leo tena.
Ila mie kwa sababu ya kubadili vyakula ili mwili usinone sana nikamuacha yeye ale mishikaki yake halafu nikapita hapo Alibasha ambapo zamani ilikuwa mikocheni sasa hivi imehamia huko mjini nikaingia hapo nikala chakula kisicho na mafuta kwa afya.

Mtoko ukaendelea ikawa ni kutembea kwa miguu mjini kote nikafika mpaka hapo penye maandishi hayo juu...unaweza kujua ni wapi hapo???????niambie kama umepajua.

Tukafika mtaa wa samora kwenye bustani tukakaa na kupiga story,ilikuwa ni usiku wa saa sita watu wamelala mjini kumejaa walinzi tu na watu wachache sana wanaorudi majumbani mwao au kutoka na magari yao,yaaani nilienjoy kuliko kwenda kwenda disco ilikuwa ni kutembea tu

Sunday, February 7, 2010

MIZUNGUKO YANGU SIKU YA JUMAMOSI...

Jumamosi yangu ilikuwa shwari sana no stress no pain...ila kujipa raha na furaha ndani ya moyo....nifanyenyeje sasa.
Huyu kaka nilikutana nae Bills aliponiona tu akaniuliza wewe ndio Dina Marios wa clouds fm nikamwambia ndio mimi eehee jamani nilikuwa nahamu ya kukufahamu....sasa pazito ni kwamba kila mtu unaekutana nae anakuomba namba yako ya simu tena tena personal hapo ndio linapokuwa tatizo.

Hapo nilienda Bills nikakutana na Marlaw nae kanenepa huyo shavu dodo hapoa alikuwa akichekacheka tu mwenyewe kama kawaida yake huwa ni mtu wakucheka na kutabasamu,sasa hivi ana albamu yake ipo mtaani inaitwa BIDII.


Mzalendo kwa Dj Venture kila jumamosi huwa kuna miduara balaa,mie nilikuwa naangalia na kutamani sana kwenda kunyongesha lakini najijua mwenyewe mzuka wangu wa mduara ukipanda nakuwa sina aibu najifanya mcheza shooo,basi ili kuepuka natizama kwa mbali.

Huyu dada anafahamiana na Anold hapo alikuwa anamsema kwa nini kila akimuomba anikutanishe nae hafanyi hivyo wakati kila leo amekuwa akimpa salamu anifikishie...na mei kiukweli Anold hakuwahi kunipa salamu za huyo dada.



Nilikutana na huyu dada ambae alifurahi sana kuniona na kunifahamu maana amekuwa msikilizaji wangu mzuri kupitia leotena tukaongea ya kuongea basi na kufahamiana.


Mie na Anold Kayanda wa Top 20 ya clouds fm.


Jumamosi hii mchana kuna shost wangu na pia dada yangu anaitwa Fausta akanipigia simu kunieleza kuwa ameleta mzigo mpya pale dukani kwake viatu,nguo za kuila aina kwa ofisi au mitoko ya usiku ,hand bag na mengineyo nikapita pale nikaona na kukupigia picha uone kama vipi unaweza kwenda.


Duka lipo Sinza Vatcan laitwa FK's Collection....waweza tembelea www.fk'scollection.blogspot.com.







Friday, February 5, 2010

HAPPY BIRTHDAY MY BROTHER GERALD HANDO...


Leo tarehe 5 january mfanyakazi mwenzangu,rafiki yangu na kaka yangu Gerald Hando ambae anasikika kila siku asubuhi saa kumi na mbili alfajiri mpaka saa tatu katika Power Breakfast ni siku yake ya kuzaliwa.Kwangu mie nakupa pongezi nyingi na kukuombea maisha marefu, afya njema,kila siku endeleza ufanisi katika kazi yako,kuwa mwenye furaha kama kawaida yako.Ni mengi ningependa kukuwish ila kubwa zaidi mtangulize mwenyezi Mungu katika kila jambo lako.Happy Birtday to you my brada..


The secret of staying young is to live honestly, eat slowly, and lie about your age. ~Lucille Ball

EVENT YA REDDS HAPO JANA PALE SAVANNA LOUNGE

Mie na Khadija Mwanamboka
Jana Redds walikuwa wanazindua muonekano mpya wa chupa ambapo walifanya event pale Savanna Lounge na tulialikwa watu kibao katika event hiyo.Ulikuwa ukifika unapewa uwa rose na kupiga picha kama hivyo

Mie niliibuka na mwanadashost Babra Hassan...hapo nilikuwa nahangaika kweli kutafuta pozi hata Shamim a.k.a Zeze anajua nilivyopata tabu.



Mimi na Babra na mishikaki ya matunda...ila jamani nimepungua kidogo si mnaona shingo inaonekana na soap dish kwa mbali.



Babra na Allen mdogo wetu mwenyewe yupo marketing hapa clouds fm.



Babra na Max


Mie na mama yangu mwenyewe Asia Idarous ambapo kesho pale move n pickatakuwa na onyesho lake la mavazi la Lady in Red akishirikiana na wabunifu wengine 16.


Mbunifu wa mitindo Khadija Mwanamboka na Geogre Kavishe wa TBL.

Thursday, February 4, 2010

USWAHILINI HATA JAMBO LA HATARI LINAWEZA KUWA KAMA SHEREHE...HAHAHAHAH

Huyu dada pichani mchana wa leo huko Magomeni kaenda kumsuta shoga yake kisa kamsema tena kwa matarumbeta kafunga mtaa na mpaka wakata viuno kawakodi kwa shughuli hiyo.
KISA:Huyu dada na huyo shoga yake walikuwa wameshibana sana mpaka nguo wakawa wanaazimana,sasa huyo shoga yake aliolewa hivi majuzi na baada ya kuolewa akawa analalamika kuwa bidada hapo pichani anamuonea wivu yeye kuolewa kiasi kwamba siku hizi kama kamchunia hata simu hampigii.Maneno yakamfikia shosti huyo hapo pichani...ndio kumkusanyia watu na kukodi matarumbeta kwenda kumsuta na kumnyang'anya microwave aliyomtunza kwenye kitchen party yake.


Shost hapo anatunzwa pesa na wapambe wake kwa shughuli nzito ya kumsuta yule dada ambae alitonywa na wapambe juu ya kasheshe inayokuja nyumbani kwake hivyo akaingia mitini mapema...

Hapo watu na mzuka wa kusuta.....


Kama kawa utadhani sherehe watu wamepagawa na msuto

Kina mama na watoto wakishangaa yanayoendeleaWenyewe wakipuliza matarumbeta yao.


Kaka wa wenyewe nae alikuwepo


Matarumbeta yamekodiwa hayo Tsh 60,000



Hapo chacha na nyonga zilihusika mwanangu.


Hapa ni nyumbani kwa shosti aliyekuwa amefatwa kwa ajili ya kusutwa lakini baada ya kutonywa juu ya kasheshe ya msuto akawa ameingia mitini na kuitelekeza nyumba yake kama hivyo kwa hiyo wasutaji wakabaki kutukana nje na kupiga tarumbeta na kucheza baadae wakaondoka...hayo ndio mambo kila jambo laweza kuwa shughuli hahahahahah!

Kama vipi sikiliza leo tena kesho na mie Dina Marios.... katika hekaheka na Gea Habib utayajua vyema yaliyojiri.

Wednesday, February 3, 2010

KWA STYLE HII UMELALA NDANI MWENYEWE UNAJUA NJE KUNA MLINZI ANAKULINDA DUUH....


Jana mida ya saa sita usiku nilikuwa napita mitaa fulani hapa Dar es salaam,nikafika nyumba flani ambayo wenyewe kwa wakati huo walikuwa wamelala ndani kimyaaaaa lakini wakiwa na matumaini kuwa wapo salama kwani nje kuna mlinzi.Lakini bwana(mmasai) huyu alikuwa kwa nje akiuchapa usingizi ile kisawasawa kama nilivyoweza kumpata...kazi kweli kweli halafu mwisho wa mwezi unamlipa kwa kazi nzito anayoifanya ya kukulinda usiku wewe na mali zako.

Tuesday, February 2, 2010

MANENO HAYO

Mitaa ya kinondoni hiyo.

JANA NILIPATA MARAFIKI WAPYA JAMANI....

Jana jioni nilikuwa pale Masaki sehemu maharufu sana kwa mishikaki ya samaki kuna binti mdogo huyo hapo kwenye picha mwenye rasta akawa anakuja na mama yake...mtoto akawa ananitabasamia mpaka akafika kwenye meza nilokaa akanisalimia na mimi nikamchangamkia vizuri mpaka mama yake akaniuliza kama twafahamiana nikamwambia hapana...basi mtoto yule akajitambulisha anaitwa Tamia.Wakaondoka na mama yake kumbe wanakaa maeneo hayo ya hapo.

Baadae akarudi akaniambia Aunty nimekuletea kaka yangu umjue...kaka mtu akajitambulisha anaitwa Tamim anatimiza miaka 13 mwezi huu tarehe 12 anasoma pale J.K.Nyerere....was so happy kiukweli kupata marafiki hawa hasa ukizingatia ni watoto.

KALENDER ZA CLOUDS FM ZITAKUWA MTAANI AU UNAWEZA KUJIPATIA KWA KUSHIRIKI KATIKA VIPINDI VYETU


LEO TENA


POWER BREAKFAST



CLOUDS FM CREW


BAMBATAA
SPORTS EXTRA

KUOSHA MACHANUO NA VITANA NI MUHIMU PIA


Ni kawaida pindi tunapochana nywele kwa kutumia chanuo au vitana kuvihifadhi na kuendelea kuvitumia pasipo kuvisafisha.Wengi tunakumbuka kutoa nywele tu basi kwenye kitana au chanuo. Lakini la msingi kumbuka kuvisafisha hasa kuviloweka katika maji ya moto mara kwa mara na sabuni ili kuyeyusha mafuta yanayokuwa yameanda katika vitana husika si mafuta tu bali hata uchafu unaokuwepo kama mba na ngozi zilizokufa.

DUNIANI KILA MTU ANA MATATIZO YAKE....


Kama umesikiliza hekaheka ya leo unawezakuwa umeshangaa lakini ni kweli,kuna kaka anakaa Kigamboni vijibweni huyu kaka anaumwa anatatizo la kula na kusikia njaa kila wakati...ana tatizo hilo kwa miezi mitano sasa anaumwa hana nguvu na anasikia njaa kila wakati.

MLO...

Kila siku anakunywa uji chupa 13 chupa inayoingia vikombe kumi na mbili ,wali kilo 3, ugali kilo moja na nusu maji vidumu 5 vya lita 5...huo ni mlo wa siku nzima masaa 24 mpaka usiku analala anaamka kula kwa njaa anayokuwa nayo...hajui anaumwa nini maana hajaenda hospitali na hana pesa ya kwenda hospitali.Anaomba msaada wa chakula na matibabu.Tunampeleka katika njia panda jumapili aweze kupelekwa hospital kupata matibabu.

Monday, February 1, 2010

ASANTE WATANZANIA KWA KUMSAIDIA HUYU MAMA KUPITIA LEO TENA...

Huyu mama mkazi wa mbagala wiki iliyopita wakati naumwa alisikika katika leo tena kupitia hekaheka ya leo na Gea Habib.Mama huyu alikuja na malalamiko mengi sana juu ya mwanaume aliye zaa nae watoto watatu kumtelekeza na kumpiga kila mara bila sababu maalum na hata kumdhalilisha mbele za watu.Mara ya mwisho mwanume huyo alimpiga sana na hata kuwapiga chini watoto aliokuwa amewabeba lakini wananchi waliingilia kati na toka siku hiyo mwanaume hajaonekana nyumbani.Nyumba waliyokuwa wakiishi akafukuzwa lakini akapata hifadhi kutoka kwa mchungaji ambae yupo pichani hapo chini.Mama huyo akadai kuwa angetamani kurudi kijijini lakini kijijini watu ambao angewategemea walishafariki.
Mama huyu alikiri kuwa ni muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi na kuomba watanzania wamsaidie kwa hali na mali kupata nguo,chakula,sabuni n.k kwani hakuwa anajiweza kwa chochote hasa ukizingatia hana shughuli ya kufanya na ana watoto wadogo 3.Kiukweli hadithi ya huyu mama ni ndefu sana na ya kuhuzunisha.


Hapa ni jana alikuwa amekuja ofisini maana kuna pesa ambayo niliifata CRDB bank kwa dada mmoja anaitwa Daina ambayo alijitolea kama msaaada kwa ajili yake.Kiukweli kina mama wengi baada ya kusikia habari ya huyu dada walijitolea sana kumpa mavazi,chakula,nguo zake na watoto,pesa,sabuni na maengine mengi na wengine kujitolea kumpa kazi ambayo atakuwa anafanya ili kujishughulisha.


Huyu ni mchungaji ambae ndio amemuhifadhi huko mbagala alikuja nae maana kulikuwa na mabegi ya kubeba hasa ya nguo na chakula


Asante sana watanzania endelea kusikiliza leo tena na tuendelee kusaidiana pia maana maisha hayatabiriki hata kidogo.

Sunday, January 31, 2010

JAMANI NILIKUWA NAUMWA..........

Naomba samahani kwa wote ambao mmekuwa mkifatilia blog hii kwa wiki iliyopita nakukuta hakuna kitu kipya ukweli nilikuwa kitandani hoi kwa malaria na typhod.Kiukweli hata kipindi sikuweza kuhudhuria maana kwa wakati huo afya yangu ilikuwa muhimu na kunilazimu kutibu maradhi na niwe na afya ya kuweza kufanya mengine ikiwemo kazi zangu na namshukuru mungu kwa sasa sijambo na ninaendelea vizuri japo si sana.

Friday, January 22, 2010

HUU NI MFANO TU..........

huu ni mfano wa weave unayoweza kusuka kwa sandra...hii nimeshonea jana kwa pembeni na kwa nyuma inaonekana ukitaka kuona kwa mbele nitafute...........hiii nimeshonea sh 55,000 but alinipunguzia bei si wajua tena mie mteja.

Thursday, January 21, 2010

MPANGO MZIMA WA KUSHONEA WEAVING MUONE SANDRA......

Huyu dada anaitwa Sandra ana saloon pale Kinondoni kwa Manyanya jengo la Mwaulanga kwa juu ...kiukweli anajua sana kutengeneza nywele hasa kushonea weaving hapo ndio penyewe.Yaani ni kazi anaifanya kwa maisha yake yote na amesomea Afrika ya kusini sio mbabaishaji.Nenda pale na style yoyote unayotaka kushonea akikuharibu njoo hapa complain..si mpigii debe ila napenda na wewe upendeze kama ukitaka kushonea weaving....anajua pia kukata mpaka raha .....

MTEMBELEE MAMA TRACY PIA KATIKA BLOG YAKE..

mambo dina...
MIMI MAMA TRACYmsikilizaji mahili wa kipindi cha leo tena na nimchangiaje mzuri wa blog yako, nakupenda nakufagilia sana. ssa mpenzi, namimi nimefungua blog yangu, ambayo ni www.beautytouchdar.blogspot.com
itangaze kupitia blog yako ili waitambue. mambo kushirikiana dina au sio???asante kwa ushirikiano


Wadau mwenzutu nae ana mambo anataka kukupa mtembelee hapo.

SINA MAPENZI TENA NA MKE WANGU...


Leo nimetumiwa msg na kaka mmoja wa Mwanza akiniomba nimshauri jambo,anasema ana mkewe wapo ndoani kwa miaka 2 lakini hana mapenzi na mkewe hampendi tena.Nikamuuliza kisa nini anasema hana sababu na wala hakulazimishwa kumuoa alimuoa akiwa na mapenzi nae kabisa lakini siku hadi siku mapenzi yamekuwa yakipotea mpaka sasa mwaka wa 2 hana mapenzi nae kabisa.Akaniomba nimshauri la kufanya...mimi nilichomuomba anipe mlolongo mzima wa maisha yao ya ndoa labda kuanzia hapo ndio naweza kujua nini kilitokea mpaka akamkinai mwenzake maana sina hakika akawa hana sababu maalumu sababu ipo ila yeye hajaiweka kichwani kama ndio sababu akiniambia ndio nitajua nimshauri nini maana kiukweli ni pazito.Labda kama wenzangu mna lakusema???

Wednesday, January 20, 2010

SASA HIVI HAKUNA VISINGIZIO TUMEEKIEWA MPAKA MASHINE KWENYE VYOO VYA BAR...

Jana katika pitapita zangu............ Hii ni mashine ya kununulia condom...kinachofanyika unaweka hela kama Tsh 100 hivi kwa juu kuna kitobo cha kuingizia pesa unazungusha kitufe fulani halafu condom inatoka kwa chini unaendelea na mambo yako...
Hayo ni maelekezo namna ya kununua

Mzigo unatokea kwa hapo....

UJUMBE WA LEO..........


Usijilinganishe na mtu yoyote hapa duniani..........................

Tuesday, January 19, 2010

INASEMEKANA HARUFU YAKO YA MWILI INAWEZA KUMVUTIA MWANAUME...

Sahau kuhusu perfume...... Chuo kimoja cha maswala ya Saikolojia nchini Uingereza kimebainisha kuwa mwanamke unaweza kumvutia mwanaume kwa harufu yako ya asili ya mwili pasipo kujipaka manukato ya aina yoyote.Inasemekana kipindi cha ovulation(kupevuka mayai kabla ya kwenda hedhi) ndio kipindi mwanamke unakuwa na kiharufu fulani cha mwili ambacho mwanaume huvutwa....haya basi kina dada tukae bila manukato kipindi hiki halafu tuone itakuwaje...lol.

Monday, January 18, 2010

HILI NALO TULIANGALIE...............

Kuna dada nilikutana nae siku ya jumamosi ana alama kibao za kuvilia damu mwilini kama kapigwa.Kiukweli nilishindwa kuvumilia nikaamua kumuuliza mwenzangu mbona hivyo kuna nini?huyo dada akaanza sasa kunieleza.
Akasema amepigwa na mumewe siku ya ijumaa,kisa alikuwa mahali anakunywa sasa kuna kaka akakutana nae akawa anamtongoza wakabadilishana namba za simu.Sasa bidada akarudi nyumbani akiwa amelewa akaenda kulala na mumewe.Usiku sana wamelala na mumewe yule kaka aliyekuwa anamtongoza akaanza kupiga simu,bidada usingizi wa pombe hasikii simu mumewe akaamka akapokea simu.Kupokea simu yule kaka anamwambia mume mpe simu mwenye simu nataka kuongea nae,mume akamjibu mimi mumewe kuna maagizo yoyote maana mke wangu kalala.Yule bwana mpiga simu akasema mie huyo mpenzi wangu duuuh mume akakata simu huku mke anakoroma kachukua mkanda akaanza kumtandika ndio bidada kushtuka usingizini kipigo kikawa kipigo.Ikibidi amwambie mumewe yule kaka alikutana nae akawa anamtongoza.Nikampa pole sana maana kiukweli alikuwa amevilia damu na yeye ni mweupe,alichonishangaza hakuvaa nguo ya kumziba ili alama zisionekane kajiacha hivyo hivyo kavaa nguo ya mabega wazi.

Sasa mimi najiuliza wewe kama mke wa mtu kwa nini unagawa namba yako ya simu hovyo?
Ok sawa umetoa namba kwa nini usimwambie huyo bwana kuwa umeolewa na asikupigie simu hovyo hasa nyakati za usiku mumeo anakuwepo?wote hatupo wakamilifu lakini tunafanyaje kuepuka matatizo kama hayo?