Friday, November 6, 2009

MAMA HUYU YUPO KATIKA WAKATI MGUMU...ILA ASANTE KWA WOTE TULIOCHANGIA JAPO KIDOGO KESHO TUNAMSAFIRISHA KWAO SHINYANGA.

Huyu mama pichani anaishi Mbagala,lakini ni mkazi wa Shinyanga kaja Dar es salaam na mumewe akimwambia wanakuja kutafuta maisha,basi wamefika mume kzi anayofanya ni ya kutapeli watu.Huyo bwana ameshatapeli watu kibao akiwaambia wampe sh laki 1 na yeye atawapa ml 5 kitu ambacho hakiwezekani.Huyo bwana katapeli wanawake kibao huko Mbagala sasa kakimbilia kamtelekeza mkewe na watoto 2.


Huyu dada ameachwa bila hata shilingi na mumewe alimwambia yeye anaondoka wala harudi tena na ataisoma namba.Ana watoto wanakula kwa msaada wa majirani hapo kabla ya kukutana na sisi.Gea Habib alikutana nae baada ya kuitwa na akina mama wa huko mbagala kwa ajili ya hekaheka ambayo imesikika jana na leo katika leo tena.




Huyo ni mtoto mdogo ambae jana alikuwa anaumwa na malaria ikabidi itolewe hela ambayo mwanamuziki Ray c alikuwa akisikiliza akaguswa na matatizo ya huyu dada hivyo akatoa pesa na kumpeleka hospital jana kwa ajili ya matibabu.

Huyo ndio mtoto wa kwanza,huyo baba jana tumempigia simu akapokea na akajibu mkewe atajijua mwenyewe yeye wala hana mpango wa kurudi,hivyo atalijua jiji...kwa sasa anatafutwa na polisi kwa utapeli.


huo mchicha juzi walipewa na mtu tu ili apike ale na mwanae na ugali yaani analala chini hana hata godoro,anatandika kanga chini ndio alale.Tunachofanya tunakusanya hela ili jumapili tumsafirishe kwao S hinyanga maana mume ndio kamtelekeza na Dar hamjui mtu hata mmoja.
wapo walioguswa na shida za huyu dada wakatuchangia kidogo chao,kesho tunamsafirisha arudi kwao Shinyanga...Asanteni sana wana Leotena,mwenyezi mungu awabariki.

Thursday, November 5, 2009

DON'T FORGET SISTERS.............


A young wife sat on a sofa on a hot humid day, drinking iced tea and visiting with her Mother. As they talked about life, about marriage, about the responsibilities of life and the obligations of adulthood, the mother clinked the ice cubes in her glass thoughtfully and turned a clear, sober glance upon her daughter

'Don't forget your Sisters,' she advised, swirling the tea leaves to the bottom of her glass. 'They'll be more important as you get older. No matter how much you love your husband, no matter how much you love the children you may have, you are still going to need Sisters. Remember to go places with them now and then; do things with them.' 'Remember that 'Sisters' means ALL the women... your girlfriends, your daughters, and all your other women relatives too. 'You'll need other women. Women always do.' What a funny piece of advice!' the young woman thought. Haven't I just gotten married? Haven't I just joined the couple-world? I'm now a married woman, for goodness sake! A grownup! Surely my husband and the family we may start will be all I need to make my life worthwhile!'

But she listened to her Mother. She kept contact with her Sisters and made more women friends each year. As the years tumbled by, one after another, she gradually came to understand that her Mom really knew what she was talking about As time and nature work their changes and their mysteries upon a woman, Sisters are the mainstays of her life.

After more than 50 years of living in this world, here is what I've learned:

THIS SAYS IT ALL:

Time passes.

Life happens.

Distance separates.

Children grow up.

Jobs come and go.

Love waxes and wanes.

Men don't do what they're supposed to do.

Hearts break.

Parents die.

Colleagues forget favours.

Careers end.

BUT.........

Sisters are there, no matter how much time and how

many miles are

between you. A girl friend is never farther away

than needing her can reach.

Wednesday, November 4, 2009

TUMEFIWA....


Mwenyekiti mtendaji wa Clouds Media Group ambayo ndio inamiliki clouds fm,choice fm,coconut fm ya zanzibar,clouds tv,primetime promotions,Bw Alex Kusaga ambaye ni baba yake mzazi na Joseph Kusaga, amefariki (jana) Pretoria ,nchini Afrika ya Kusini ambako alipelekwa kwa ajili ya matibabu.
Kwa taarifa zilizopatika ni kwamba msiba upo nyumbani kwake Mbezi-Beach karibu na Giraffe Hotel.
Aidha kwa taarifa zaidi tutaendelea kufahamishana kadiri ya zitakavyokuwa zinatujia.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN
Leo sina lakuweka naenda kwenye msiba,asanteni.

Tuesday, November 3, 2009

SAFARI HII SIDHANI KAMA ELIZABETH ATAPONA,NIMEPOTEZA IMANI KABISA NA HIVI WATANZANIA HATUPENDI KUPIGA KURA...

Elizabeth akiwa katika pozi na D'banji mwanamuziki kutoka Naigeria alipowatembelea weekend iliyoisha.Elizabeth yupo up for evection this week akiwa na Emma kutoka Angola na Nkena kutoka Naigeria.
Mwamuziki Kerri Hilson kutoka nchini Marekani aliwahi kutembelea pia jumba la Bba4 na Elizabeth kupata nafasi ya kupiga nae picha na kumshikisha bendera ya nchi yetu.


Awali walikuwa Mzamo,Emma na Nkena lakini Edward ambae ni HOH akamtoa Mzamo na ku mswap Elizabeth kama revenge baada ya Elizabeth kufanya hivyo hapo awali kwa kumswap pacha wake Edward.... Erastus na akatolewa humo ndani,hivyo amekuwa na kinyongo na ameamua kulipiza kisasi anasema pacha wake hakuwa mtu mbaya na angefurahi mpaka sasa kama angekuwepo.........duu tunalo jamani tumpigie kura mwanadashost... Andika kwenye simu yako vote Elizabeth kwenda namba 15726 kwa mitandao yote ya tigo,vodacom na zain....kiukweli nahisi bidada anatoka this sunday yaani sielewi.

Usain Bolt....Alipotembelea nchini Kenya..........

Alizaliwa tarehe 21 August 1986 (1986-08-21) kwa sasa ana miaka 23 Ni mkimbiaji wa mita 100_ambae inasemekana ndio the fastest man on earth kwa sasa baada ya kuweka record ya kukimbia mita 100 kwa sekunde 9…RECORD AMBAYO HAIJAWAHI KUWEKWA NA MTU YOYOTE na kuvunja record yake mwenyewe ya nyuma ya sekunde 14…
MWANARIADHA huyu kutoka Jamaika ambae anashikilia medali ya dhahabu ya kwa mara tatu katika mashindano ya olyimpic…ijumaa ya tarehe 30 october ALITEMBELEA NCHINI Kenya kwa ajili ya kuzindua asasi isiyo ya kiserekali kupitia Zetz Foundation inaliyopewa jina la Long Run.Mradi huo umezinduliwa kwa ajili ya kulinda mazingira.Jumatatu jana Usain Bolt alitembelea Kenya Wildlife Service (KWS) ambapo alipewa zawadi ya duma mtoto aliyekabidhiwa na Zetz Foundation…ambae amepewa jina lake…

MWANAUME ANAPOKUNYANYASA UKIMUACHA ANAKUFANYIA VISA,HATAKI AKUONE NA MWANAUME MWINGINE WAKATI YEYE ANA MWANAMKE....


leo kwenye hekaheka tulikuwa da dada mmoja mkazi wa Keko hapa Dsm,amelalamika sana juu ya mwanaume aliyewahi kuwa nae kama mchumba na alishamlipia mahari lakini akamshindwa kutokana na tabia ya mwanaume huyo ya umalaya na kumpiga.Baada ya kuachana lakini kwa mbinde maana mwanaume alikuwa hataki kuachwa basi mwanaume kila akimuona huyo dada na mwanaume mwingine anazusha ugomvi balaa,wakati huyo mwanaume ana mwanamke mwingine na amezaa nae.Huyo dada anasema amechoka kweli na hana amani na maisha yake mpaka wanaume wanamuogopa kisa watafanyiwa fujo na bwana....kiukweli dada wa watu yupo kwenye wakati mgumu kabisa...

BAADHI YA MAONI YA SMS ZA WASIKILIZAJI
1.Huyo mkaka bado anampenda huyo dada,anachotakiwa kufanya huyo dada ahame mji...awe mbali na huyo bwana.
2.huyo dada aende kwa mumewe si kalipiwa mahari.

3.Yaliyomkuta huyo dada hata mimi yalishanikuta,mie nilikuwa naviziwa njiani napigwa hadi basi,Aisha.

4.wivu tu unamsumbua huyo mwanaume,Khalid
5.wanaume ndio zao anataka kukuacha wewe tu wewe ukimuacha atakukosesha raha mpaka basi sijui wakoje,mie yashanikuta hayo..Sophy..
6.Leo mmenikumbusha mbaaali na hiyo hekaheka ya huyo mwanadada anaesumbuliwa na jamaa yake wa zamani kisa hataki au (cjui niseme hajui kuachwa) Dina wanaume wengi ndo walivyo. Mi mwenzio nilitaka kuuliwa nini huyo anapigwa. Achilia mbali kupigwa, kashfa, na kejeli. Mi niliingizwa kwenye gari na kuendeshwa kama napelekwa kuzima moto. Ni nje ya mji nikapelekwa porini kabisa gari ikazimwa na taa za gari zikazimwa yaan huko labda nyoka tu ndo wangetuona na uhakika ningeuliwa hakuna ambae angejua au ingechukua muda mrefu. Akanipiga na kuanza kunikaba kwa kamba, mi nipo kiti cha mbele yeye akiwa kiti cha nyuma. Nikaishiwa nguvu Dina. Huku naambiwa wewe si hunitaki sasa ngoja nikuue. Utaamini mtu huyo nimezaa nae? Alikuwa hafikirii kabisa kuhusu baby boy wetu. Dina unajua nini kiliniokoa siku hiyo, baada ya kuomba sana asiniue nikashindwa, nikawa nimekubali kufa. Kilitokea kishindo kikubwa sanaambacho hadi leo sijui kilikuwa nini wote tukawa tunaogopa. Jamaa alishuka kwenye gari na kuingia kwa dereva na kuwasha gari na kunirudisha aliponitoa. NI MUNGU TU ALINIOKOA

Monday, November 2, 2009

MITOKO MINGINE WEEKEEND HII ILIYOISHA.....RED CARPET MACHOZI KWA LADY JAYDEE...

Gadner G.Habash akiwa na wife wake Lady Jaydee...walituandalia usiku wa ki red carpet pale Zong hua ijumaaa iliyopita na kutupa burudani ya aina yake sambamba na machozi band.
Mie nilikuwepo niliingia hapo mida ya saa saba na nusu usiku nikitokea katika show ya uzinduzi wa jahazi modern taarabu hivyo nikachelewa kupiga picha kwenye red carpet jamani...hapo nipo na mashost zangu wa leo tena,suzy mwenye banio kubwa kichwani...hahahah mwanamke kujichora hena,na zamaradi katikati...kwani mie si mwanijua nimekaa wapi?nimevaaje?lol hahahahaha


Jaydee akiwaweka juu mashabiki wake siku hiyo,rangi iliyotawala ni nyekundu...thats my favourate colour...ikipita week sijavaa au kuweka kitu chekundu mwilini naona sijajitendea haki....picha za jahazi zaja.

Sunday, November 1, 2009

MITOKO MBALI MBALI HII ILIKUWA PARTY KWA SHYROSE BHANJI.........


Mwenyewe nilikuwa nipo nimejaa tele...ilikuwa party ya kumpokea Shyrose akitokea mapumziko Marekani



Mie na Shyrose tuki show love na picha ya ukumbusho....





Mwanadada Khadija Mwanamboka pia alikuwepo (i really like her)ana kitu very special nitawaambia siku moja about her,na Reuben Ndege.


Vijana wa mjengo kama kawaida walikuwepo kufurahi pamoja na Shyrose Reuben Ndege,Sade,Dj Fatty na Anold Kayanda.


Kushoto kwako huyo anaitwa Suzy,Shyrose na mimi mwenyewe alliyrsimama na kivazi cha blue Zamaradi.....



Anold buzy anakula.mie na Jaffarah tupo katika pozi la picha.

Friday, October 30, 2009

SORRY.........MAJUKUMU NI MENGI....

MAONI NA MASWALI YA WADAU
1.DINA UCSAHAU ZILE PICHA ZA JAHAZI,MANA UZINDUZI NDO LEO SAWA MAMAA.
2.Alafu Dina mbona hujanijibu kama clauz Tv imeshaanza kuwa hewani,alafu utuwekee picha za Gerald hando na babla.

3.dina mambo?Hakikisha unapost picha za leo ukiwa mzigoni na wana jahazi, maana mimi hata leilah simjui jamani,its mariam

4.Mi naungana na Mariam,n kweli Dina uzipost hizo picha za jahazi,nacie tuciobahatika kwenda angalau tuinjoi kupitia kwako,sawa mamaa.Asia Alawi


MAJIBU YANGU DINA KWENU
clouds TV ipo tayari na mtambo umeshawashwa wapo kwenye kuset vizuri mitambo,picha ya Gerald na Babra nitaiweka iwapo wenyewe wataniruhusu ila najua hawata kataa sikilizia next week,pia ntajitahidi kupiga picha leo nikiwa na Mc uzinduzi wa album ya jahazi modern taarabu pale Dimond jubelee karibuni wale mtakaokuja,ambao hamtakuja nitawawekea picha,,,,Mariam nitajitahidi nipige picha na leyla niiweke umuone
Mwisho....nawapenda na nawatakia mengi ya heri katika weekend yako
''BECOMING NUMBER ONE IS EASIER THAN REMAINING NUMBER ONE"

GRACA MACHEL................

Hapo juu nimetumia jina lake maarufu zaidi ......... Mwanamama huyu ana bonge la historia ambalo hakuna mwanamke mwingine amewahi kulifanya hapa duniani .....can u tell me??na kama yupo ambae amefanya alichofanya Graca pia niambie..

HILI NIMETUMIWA. NA MDAU...ETI RAHA JIPE MWENYEWE!!!

Kama Roho yako inapenda Gari la Kifahari …..
Why are you going for the expensive House !!

Na Kama Roho yako itapenda kuwa na DSTV …
Why should you build a good house while you have somewhere to lay down your ribs !!

Satisfy your Soul First and your Soul will satisfy you in turn !!




Thursday, October 29, 2009

STORY YA WANASIASA

Wanasiasa 40 walipata ajali mbaya sana porini,na baada ya ajali hiyo alitokea mkulima mmoja na alipoona hivyo alichimba shimo kubwa na kuwazika wote kwa pamoja.Baadaye polisi walikuja eneo la tukio na kumkuta huyo mkulima na kuanza kumhoji kuhusiana na ajali hiyo pamoja na maiti.
na mahojiano yalikuwa hivi:-
Polisi :- Uliona ajali jinsi ilivyotokea?
Mkulima :- Hapana, nilikuta imeshatokea na maiti zimezagaa..
Polisi :- Zipo wapi maiti?
Mkulima :- Nimezizika
Polisi :- Una uhakika wote walikua wamekufa?
Mkulima :- Kuna wengine walikuwa wanalalamika kwamba hawajafa lakini si unajua wanasiasa walivyo waongo!!!mi nikajua tu wanadanganya nikawazika wote....

Thanks to Mdau Rose Maduhu

KUNA VITU VINGINE NI VIDOGO SANA LAKINI NI MUHIMU SANA KUWA NAVYO NYUMBANI............


Amekuja mgeni nyumbani kwako,kwa ukarimu wako unampa kinywaji labda soda au beer...mnaanza kutafuta opener ya kufungulia hiyo soda haionekani au huna kabisa.Unakaa mbele ya mgeni nakuanza kufungua hiyo soda kwa meno au hiyo beer huku ukisema ''samahani bwana opener ilikuwepo watoto wameichezea tu sasa haionekani wacha nikufungulie na meno" hicho ni kisingizio chako na vingine vingi tu...hako kadude ni kadogo lakini kana nafasi yake hapo nyumbani inawezekana unayo but iweke mahali inapoonekana ili usijitie aibu mbele ya mgeni,mgeni atakuchunia tu lakini moyoni amekereka..kumfungulia na mdomo ina husu???....mie ninako tena kale kenye sumaku nimekanasisha kwenye fridge kabisa....

Wednesday, October 28, 2009

FIESTA 2009...DAR ES SALAAM...ONE LOVE!!!


Itakuwa tarehe 7 november pale uwanja wa chuo cha posta
msanii Busta Rymes kutoka nchini Marekani atakuwepo na wengine wengi wa hapa nyumbani.......karibuni sana.

Tuesday, October 27, 2009

WEE KWANI KABILA GANI?

Ni kawaida sana unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza kukuuliza "hivi wewe ni kabila gani"nauliza tu kwa wewe kujua kabila langu ina kupa faida gani?why tunauliza kabila la mtu ili tuhakiki nini kwa mtu huyo?nilikuwa najiuliza mwenyewe tu lakini naomba unisaidie?
mama wa kimakonde....huyu ukimtazama tu unajua ni kabila gani.

MUME ANAPOMUOMBA MKE KUFANYA TENDO LA NGONO KINYUME NA MAUMBILE...


Nimekutana na wanawake wengi sana ambao wapo ndoani wengi wakilalamika kwa tabia mbaya ya waume zao kutaka kufanya nao mapenzi kinyume na maumbile,wengine wakilalamika kuchoshwa na tabia ya waume zao kuwaingilia kinyume na maumbile,sometimes najiuliza kwa nini unakubali mwanaume akufanyie hivyo kisa ni mumeo?ukikataa atakuacha?anakushinikiza kiasi huwezi kukataa?anakubaka?kila mtu huwa na hadithi yake....na mimi si walaumu sana maana siwezi jua kama wakinipa kiatu chao nitaweza kukivaa.

MUHIMU.
Kesho katika leo tena kwenye hekaheka ya leo na Gea Habib,msikilize dada aliyeolewa kwa ndoa kabisa mkazi wa mkoa wa Tanga,akakaa ndoani miezi 6 akaondoka kwa mume baada ya mume kuanza kumuomba penzi kinyume na maumbile,dada anasema alimwambia mwanaume kama haridhiki na yeye kama mwanamke kuliko ampe kinyume na maumbile bora waachane,mdada alienda kuwaambia wazazi wake...wazazi wakamwambia kama ni hivyo bora muachane tu. Mwanaume hakutaka kutoa talaka lakini aliitoa kinguvu baada ya mshikemshike wa hapa na pale pls kesho usikose.

Monday, October 26, 2009

TUNAPOHAMIA KWENYE NYUMBA TULIZOJENGA?AU YA KUPANGA HUWA TUNAUTARATIBU WA KUFAHAMIANA NA KUJITAMBULISHA KWA MAJIRANI ZETU TULIOWAKUTA?

Tulikuwa tukizungumza na wana leo tena leo kwamba ukihamia nyumba mpya aidha umejenga,umepanga,au umenunua ni kwako..unahamia na kuwakuta majirani wapya kuna ulazima wa wewe kujitambulisha kwao wajue kama kuna jirani mpya kahamia?
Hizi ni baadhi ya msg nilizopata
1.Kuna shoga yangu alihamia kwake akaenda kwa jirani kujitambulisha mbona alikoma,aliambiwa atoke Mzee na mkewe wamelala,Doris wa Mbezi.
2.Huo ni utaratibu mzuri hata kama sio nyumba zote lakini atleast zile za karibu yako,ukikaa kimya kesho unaweza pata tatizo halafu wakakuchunia,Cathy wa Tanga

3.Utaratibu huo wa kujitambulisha kwa majirani labda uwe umejenga kwako,kama unapanga usipoangalia unaweza julikana Dar nzima,mama Najma wa Mburahati.

4.Mie nahisi ni wachache ndio hufanya lakini mie kuna sehemu tulihamia wenyeji wetu ndio walitufata kutukaribisha maana waliona ni wageni lakini sisi tulinyamaza,Rose SK.

5.Dina maisha ya siku hizi hakuna utaratibu wa kufahamiana na majirani zaidi ni kukutana mtaani,Heleni Msumba wa Moshi.

pongezi kwa shost wangu Fide kwa kujenga nyumba hiyo hapo pichani maeneo ya njiro huko Arusha...hongera sana nakumbuka vile tulivyokuwa tukipanga wenyewe maisha kuhusu kununua viwanja,tujenge tuwe na nyumba zetu and so many.....safi sana mwenyezi mungu akuongezee zaidi ya hapo..

GUBU LINAPOZIDI KWA MUME AU MKE NINI MADHARA YAKE??

Aunty Sadaka mwenye kilemba kwa wale msiomfahamu....tunakuwaganae kwenye leo tena kila jumanne kuongelea mambo kibao ya maisha.............
Tuungane na Aunty Sadaka leo katika leo tena mida ya Saa tano na dk 45...Gubu kwa mume na mke madhara yake ni yapi katika mahusiano yao ya ndoa??usikose...

KWIKWI.........Hiccuping

Mara nyingi mtu ukishikwa na kwikwi kuna mengi una shauriwa ufanye ili kumaliza kwikwi......utaambiwa mpaka mtu akushtue ukistuka basi kwikwi inakwisha...au weka kiuzi ambacho umekilowesha na mate kwenye paji la uso.....
Na pia huambiwa kunywa maji....maji unakunywaje ili kumaliza kwikwi
1.kama umebanwa na kwikwi kunywa maji safi na salama glasi nzima pasipo kupumzika mpaka maji yaishe kwenye glasi.
2.ukimaliza shusha pumzi,baada ya hapo bana pumzi kwa sekunde 15....au angalau 12...baada ya hapo kwikwi itakuwa imeisha....iwapo bado haijaisha rudia step izo tena na itakwisha.

Jana nimeielezea kwenye kipindi kuna mama akanitumia msg kwamba anamwaka sasa ana kwikwi ambayo haijawahi kuisha kabisa nikamshauri aende hospitali akamuone daktari ili aweze kupata ushauri wa kitabibu zaidi..maana kwikwi mwaka!!!

Friday, October 23, 2009

WEEKEND NJEMA WAPENDWA.............

Kiukweli ukiwa unanenepa nikama mchezo tu lakini ukishanenepa wakati wa kupunguza mwili si mchezo...nimekaa ofisini nikawa naangalia picha zangu za miaka mitatu iliyopita mmmh sina la kusema zaidi ya kukazana mazoezi....lol..



Mie nawaombea mema na ya kheri katika kipindi cha mapumziko ya mwisho wa wiki...tukikutana kwenye mitoko sawa lakini nafikiri weekend hii nitaitumia zaidi nyumbani na pia kusalimia marafiki...nina rafiki zangu wawili Fide na Robi wamejifungua hivyo nitaenda kuona watoto...


NOTE:
1.Be who you are and say what you feel because those who mind don't matter and those who matter don't mind.
2.. Always put yourself in the other's shoes. If you feel that it hurts you, it probably hurts the person too.
3.Throughout life people will make you mad, disrespect you and treat you bad. Let God deal with the things they do, cause hate in your heart will consume you too.
4.If today was perfect there would be no need for tomorrow.
5.You have enemies? Good. That means you've stood up for something, sometime in your life.
6.Nowhere on your birth certificate did it say life would be fair.
7.Not all scars shows. Not all wounds heal. Sometimes you can't see, the pain someone feels.
I LOVE YOU ALL...HAVE A LOVELY WEEKEND

MC BABU AYUBU.........KAZI KWELIKWELI


Huyu bwana nilikuwa nae leo kwenye kipindi cha leo tena....anaitwa Mc Babu Ayubu amekuwepo katika sanaa ya uigizaji kwa muda mrefu lakini yeye amekuwa akiiga sauti za watu mashuhuri katika nyanja nyingi kiburudani,kisiasa n.k....mimi nilikuwa na mengi ya kuongea nae kubwa zaidi ni style yake ya kutembea na chupa ya maziwa ya mtoto kama unavyomuona kwenye picha.Chupa hiyo anabebea soda,bia,maji na ulevi wowote atakaokuwa anautumia kwa wakati huo na hutembea nayo mkononi akinyonya kama mtoto....leo alikuja chupa ikiwa na maji,nilipomuuliza kwa nini akanijibu ni katika kuonekana tofauti na kutafuta utambulisho wake kama msanii...duuh!!kazi kwelikweli.

SAMAKI WA KUCHOMA.........

Nimekaaa nikajifikiria sana baadae nikaamua kula samaki wa kuchoma nikamuagiza hapo Kawe club karibu na hapa ofisin...ni samaki wa kuchoma kwenye foil....anachomwa akiwa mbichi kabisa tena wa leoleo.....na ndizi yangu moja ....hiyo nyingine ilinishinda akala Zamaradi....kwa sasa nipo fresh tu nimekunywa na maji ya kutosha nashukuru sana kwa pole zenu mbarikiwe...kuna mdau kasema si nife tu au ndio ukimwi umenianza,mie nasema inshalah tu kwamaneno yake Mwenyezi Mungu wetu sote wabaya kwa wazuri wala sitakuhukumu kwa kauli yako maana anaetuhukumu ni aliyetuweka duniani nna nini mie Dina kukufumba wewe mdomo??just remember Life is too short to waste time hating anyone... Don't hate others

Jamani msijesema Dina aliangusha uma halafu akauokota na kuendelea kuutumia.........hapo kilikuwa kitu cha mkono....

NAUMWA...........


JAMANI LEO TOKA ASUBUHI......................naendesha ile mbaya jana usiku sijala chakula nyumbani nimekula restaurant moja ipo maeneo ya sinza basi toka asubuhi tumbo linauma ghafla shughuli ikaanza hapa nakunywa maji tu hata kula sitamani ngoja niangalie kitu cha kula kinachoeleweka maana................

Wednesday, October 21, 2009

KILA SIKU MSHUKURU MUUMBA WAKO KWA KUKUWEKA SALAMA KWANI HUWEZI JUA YA KESHO.........


Anaitwa..Jacqueline "Jacqui" Saburido amezaliwa December 20, 1978 in Caracas, Venezuela...Ni muhanga wa ajali ya moto uliomuunguza baada ya kupata ajali ya gari iliyosababishwa na dereva mlevi ..amekuwa akifanya kazi kupinga na kuelimisha madhara ya kuendesha ukiwa umelewa....pichani hapo juu ni wakati akiwa hajakumbwa na masaibu...


Hapa katika picha ni alivyokuwa zamani na alivyo sasa ....hembu fikiria ni mtoto wa pekee katika familia ya Rosalia na Amadeo Saburido....ajali ilitokea September 19, 1999 wakati akitokea kwenye party ya rafiki yake akiwa na marafiki zake Laura Guerrero, Johan Daal na Johanna Gil,wakapewa lift na mwanafunzi mwenzao Natalia Chpytchak Bennett.
wakiwa njiani kijanaReginald Stephey aliyejuwa na umri wa miaka 17-wakati huo tena mwanafunzi alikuwa na yeye njiani akirudi nyumbani akitokea kwenye party tena akiwa anaendesha gari amelewa na kugongana na gari ya kina Jacque.... Guerrero na Bennett walikufa hapohapo,Gil na Daal waliumia kiasi tu na Jacque miguu yake kukwama ndani ya gari na kushindwa kutoka na..baadae gari kuwaka moto kwa dk 45 akiwa bado amekwama kwenye gari na kuungua asilimia 60 ya mwili wake.


Mungu mkubwa alikuja kutolewa baada ya ammbulance kufika...lakini akiwa ameungua na kupoteza pua,masikio,nywele,masikio,macho,na maeneo mengine mengi..katika maisha yake ameshafanyiwa upasuaji zaidi ya mara 40.

Jacqueline Saburido alitokea katika kipindi cha mahojiano cha Oprah Winfrey Show mwezi November 17, 2003...na oprah kumtambulisha kama "a woman who defines survival."...kijana aliyesababisha ajali alipona na wakati wa kesi mahakamani Jacquline alimwambia "pamoja na kwamba umeniharibia maisha nimekusamehe kabisa"..japo alikuja kutumikia kifungo cha miaka 7.
*****Mshukuru mungu kwa kila jambo...hesabu baraka anazokujaalia leo si na kulalamika kila wakati,ukisoma kisa cha huyo dada unafikiri wewe una mazuri yapi kumzidi yeye mpaka leo hii mungu amekujaalia mengi?waheshimu na wengine jeuri haisaiidii kitu mlimwengu,chuki kwa wengine ni hasara kwako inaashiria hujipendi..upendo huanzia kwako mwenyewe ndio uweze kuwapenda wengine...nawapenda sana.

NI KWELI HOST WA SASA HIVI WA BBA4 REVOLUTION HAVUTIII??

Anaitwa IK Osakioduwa..........
akiwa ni kijana mwenye kipaji, mzungumzaji na mchangamfu raia wa Nigerian television star IK Osakioduwa ambae tayari alisha julikana ndani ya Africa. An Economics graduate katika chuo kikuu cha Lagos ambae alianza siku nyingi kazi hii ya utangazaji huko Naigeria katika kipindi cha 'Wild Child' katika radio station Rhythm FM 93.7, IK baadae alihamia ktk tv…Sasa hivi ni mtangazaji wa M-Net's flagship Afro-chic lifestyle program Studio 53 akiwa na kina Gaetano Kagwa ,na ameshaonekana katika vipindi vingine vya M-Net lakini cha Nigerian game show Temptation na pia the stand-out stand-up series Comedy Club: Live in Lagos.....ila watu wengi ambao nimekaa nao wanaonekana kummiss sana Kabelo ambae alikuwa Host wa BBAzilizopita....ni kweli kijana hajanoga au ni mazoea tu yetu sisi...
Kabelo Ngakane.....mtangazaji katika kituo cha television cha channel o hukohuko Afrika ya kusini......ambae amekuwa host mara kadha katika BBA zilizopita.......