Huyu mama pichani anaishi Mbagala,lakini ni mkazi wa Shinyanga kaja Dar es salaam na mumewe akimwambia wanakuja kutafuta maisha,basi wamefika mume kzi anayofanya ni ya kutapeli watu.Huyo bwana ameshatapeli watu kibao akiwaambia wampe sh laki 1 na yeye atawapa ml 5 kitu ambacho hakiwezekani.Huyo bwana katapeli wanawake kibao huko Mbagala sasa kakimbilia kamtelekeza mkewe na watoto 2.
Huyu dada ameachwa bila hata shilingi na mumewe alimwambia yeye anaondoka wala harudi tena na ataisoma namba.Ana watoto wanakula kwa msaada wa majirani hapo kabla ya kukutana na sisi.Gea Habib alikutana nae baada ya kuitwa na akina mama wa huko mbagala kwa ajili ya hekaheka ambayo imesikika jana na leo katika leo tena.
Huyo ni mtoto mdogo ambae jana alikuwa anaumwa na malaria ikabidi itolewe hela ambayo mwanamuziki Ray c alikuwa akisikiliza akaguswa na matatizo ya huyu dada hivyo akatoa pesa na kumpeleka hospital jana kwa ajili ya matibabu.
Huyo ndio mtoto wa kwanza,huyo baba jana tumempigia simu akapokea na akajibu mkewe atajijua mwenyewe yeye wala hana mpango wa kurudi,hivyo atalijua jiji...kwa sasa anatafutwa na polisi kwa utapeli.
huo mchicha juzi walipewa na mtu tu ili apike ale na mwanae na ugali yaani analala chini hana hata godoro,anatandika kanga chini ndio alale.Tunachofanya tunakusanya hela ili jumapili tumsafirishe kwao S hinyanga maana mume ndio kamtelekeza na Dar hamjui mtu hata mmoja. wapo walioguswa na shida za huyu dada wakatuchangia kidogo chao,kesho tunamsafirisha arudi kwao Shinyanga...Asanteni sana wana Leotena,mwenyezi mungu awabariki.
_-_Two_Sisters_(1901)%5B1%5D.jpg)



























