Kama unakumbuka nilishakuletea historia ya Mwanamakuka,mwanamama wa kinyamwezi mjasiriamali wa kwanza katika pwani ya Afrika Mashariki.Aliishi karne ya 18 ambae alikuwa akisafiri katika misafara ya kibiashara wakati huo ilikuwa ya mbadilishano.Akibeba vyungu,asali,pembe za ndovu,mtama,mahindi,uwele,chumvi,samaki wakavu n.k
Biashara yake alikuwa akiifanya pia na wakoloni ambao wakati huo walikuwa waarabu.Kuelekea siku ya wanawake duniani tunataka kinamama wajasiriamali wa sasa wa karne ya 21 wamjue huyu na wafuate nyayo zake.Na pia kuchukua fursa ya kuwashika mkono wale waliokwama ndio maana kuna hili shindano la NYAYO ZA MWANAMAKUKA.Mshindi atazawadiwa siku ya wanawake duniani 8th march pamoja na mshindi wa pili na wa tatu.
No comments:
Post a Comment