Tuesday, April 3, 2012

DADA JUDY NA MWANAE

Ni dada anaenisaidia kazi za nyumbani.Mwanae ana miezi minne sijawahi kushinda nae weekend hii nikawepo.Naingia jikoni tu namkuta anaosha vyombo halafu kambeba kamuweka juu karibia na sink.
Analia huyooooooooo,yaani muda wote anapenda kubebwa au aone mtu jirani mbali na hapo ni kilio tu.

14 comments:

  1. Hello Dina,pole na majukumu kuhusiana na dada bora wa nyumbani inakuwaje nihabarishe kwani wa kwangu yuko vizuri sana na nampenda sana

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe kama bosi wake utatakiwa kuandika barua kutuambia kwa nini dada wako wa kazi hapo nyumbani ni bora?kwa nini azawadiwe?je upo tayari aendelezwe ili aweze kupiga hatua nyingine zaidi ya hiyo katika maisha yake?

      Delete
    2. Hi Dina pole kwa kazi,najua nakuchosha na maswali ila itabidi kwani mimi huwa napenda sana kufungua blog yako na nimejifunza mambo mengi kupitia blog yako
      Swali langu ni hili barua nai address kwa nani?
      isitoshe mimi niko mikoani au hii ni kwa ajili ya wakazi waishio Dar tuu?? pls naomba nijulishe niko Arusha.

      Delete
  2. Mnunulie Baby walka dina anamkalisha inaenda yenyewe na inavikengele atakua busy kulilo anavyomuweka juu ya meza ya jikoni ataanguka Dina. Kwani wakati mwingime binadamu hupitiwa bora nusu shari dina -

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sawa ndugu yangu umesomeka tutajitahidi kwa hilo.

      Delete
  3. OYAA KUWA MWANGALIFU MAZINGIRA YA JIKONI KWAKO SI MAZURI KWA MTOTO VITU KAMA SABUNI, VISU CHEMICALLS , VIKO KARIBU SANA NA MTOTO HIZO ZOTE NI HAZZARD NAJUWA MNAWEKA KARIBU KURAHISISHA KAZI ZENU ILA HAMJUI AT THE SAME TIME U HAVE CREATED A SHORT CUT KWA MTOTO KUONDOWA UHAI WAKE , HUKU KWETU AKIJA HEALTH VISITOR AMKUTE MTOTO HAPO AU AONE HIYO PICHA NINAWEZWA KUNYANG'ANYWA MTOTO KABISA NA SERIKALI .

    ReplyDelete
    Replies
    1. Asante kwa ushauri ntamwambia dada awe mwangalifu maana sio kwamba naishi nae.
      Ni dada anaekuja kufanya usafi asubuhi mpaka saa sita mchana anakwenda kwao.Mie sina familia ya kusema nahitaji dada wa kazi wa kulala kabisa.Hayo ni mazingira ya nyumbani kwangu hata kabla hajapata mtoto.Kubwa ntamwambia awe mwangalifu kwa mtoto maana muda mwingi sipo nyumbani yeye akiwepo labda jumamosi tu na jumapili ni siku ya yeye kuwa off haji.

      Delete
  4. Dinna hii inazidi kuprove hisia nilizonazo juu yako kuwa una utu sana na huruma ndo maana unaweza kaa na housegirl mwenye mtoto ukawalea wote.there is something in you frankly speaking. i love you, i love the way you handle issues,i love the way you educate us through your blog, you are my role modal, i wish to see you and talk to you live one day!

    ReplyDelete
  5. Dina unatisha na unachonifurahisha roho yako ni nzuri ukitaka kumjua mtu maongezi yake tu MUNGU wangu ninae mwabudu akubariki sana. Nakutakia mapumuziko mema ya sikukuu.SOPHIA.

    ReplyDelete
  6. Dina mi napenda ua style. Tunaendana sana.

    ReplyDelete
  7. hongera sana ndugu yangu kwa moyo mzuri mwaya wa kumlea dada na mtoto wake ni wachache sana wenye moyo huo

    ReplyDelete
  8. Yeah ni mwajiri bora kati ya waajiri wachache wanaokubali msaidizi mwenye mtoto pia una moyo wa huruma kwani nakufuatilia kwenye vipindi vyako sijawahi kukutana nawe au kupata info kwa mtu yeyote nahisi tu basi nakuomba msaidie huyo dada japo apate ujuzi wa cherehani tu aweze kukuza kipato na kuweza kumtunza mwanae na kumsomesha mwanae sorry kama nitakuwa nimekukwaza Mungu akubariki nakupenda sana

    ReplyDelete
  9. ubarikiwe san dina

    ReplyDelete