Thursday, July 17, 2014

MPANGO WA DADA DINA CARES UNAKARIBIA UKINGONI

Napenda kuwashukuru wote wanaoendelea kuchangia chochote katika mpango huu wa dada dina cares.Ambao tunakusanya pesa za kununua vyakula,sabuni za kufua na kuoga,mafuta ya kujipaka,dawa za meno,vifaa vya shule,neti za mbu n.k
NAMBA ZA KUCHANGIA NDIO HIZI 0759 789863 na 0657 795654 ukituma zitaonyesha jina Halima Temu.Usiogope huyu ni dada amejitolea kunisaidia katika hili hivyo yeye ndio atakuwa akikusanya hela.Tutahudumia vituo vya watoto yatima vilivyopo hapa Dar es Salaam.Vituo vitakavyohudumiwa ni mwandaliwa kiko mbweni,house of hope kiko mabibo,veterani kipo temeke,zaidia kipo sinza na sifa kipo bunju.Kama bado karibu sana kuchangia.Kama una vitu pia uanakaribishwa kwa kuvifikisha ofisi za clouds fm mikocheni.

No comments:

Post a Comment